UTT AMIS yadhamini mkutano wa Maofisa Habari Serikalini

Waziri Mkuu akifungua kikao kazi cha Maofisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanyika Mwanza katika ukumbi wa Benki kuu. Katika ufunguzi huo amewaasa maafisa hao kutoa habari sahihi na kwa wakati ili wananchi wafahamu wananufaikaje na taasisi mbalimbali zilicho chini ya Serikali.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akikabidhi cheti cha shukrani Ofisa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Martha Mashiku, kwa kudhamini kikao Kazi cha Maofisa Mawasiliano wa Serikali kilichofanyika Jijini Mwanza.